Zaburi. 110. Zaburi ya Daudi. Bwana amwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa mahali pa kuweka miguu yako.” Bwana ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni; utatawala katikati ya adui zako. Askari wako watajitolea kwa hiari katika siku yako ya vita. Ukiwa umevikwa fahari takatifu, kutoka tumbo la mapambazuko utapokea umande wa ujana wako. Bwana ameapa, naye hatabadilisha mawazo yake: “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.” Bwana yuko mkono wako wa kuume, atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake. Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga na kuwaponda watawala wa dunia nzima. Atakunywa maji katika kijito kando ya njia, kwa hiyo atainua kichwa chake juu.