Zaburi. 136. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema. Mshukuruni Mungu wa miungu. Mshukuruni Bwana wa mabwana: Kwake yeye pekee atendaye maajabu makuu, Ambaye kwa ufahamu wake aliziumba mbingu, Ambaye aliitandaza dunia juu ya maji, Ambaye aliumba mianga mikubwa, Jua litawale mchana, Mwezi na nyota vitawale usiku, Kwake yeye aliyemuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, Na kuwatoa Israeli katikati yao, Kwa mkono wenye nguvu ulionyooshwa, Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu, Na kuwapitisha Israeli katikati yake, Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu, Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa, Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu, Naye aliwaua wafalme wenye nguvu, Sihoni mfalme wa Waamori, Ogu mfalme wa Bashani, Akatoa nchi yao kuwa urithi, Urithi kwa Israeli mtumishi wake, Aliyetukumbuka katika unyonge wetu, Alituweka huru toka adui zetu, Ambaye humpa chakula kila kiumbe. Mshukuruni Mungu wa mbinguni,