Habakuki
1Habakuki1 1:1Neno alilopokea nabii Habakuki.
Lalamiko La Habakuki
2 1:2Ee
Bwana, hata lini nitakuomba msaada,
lakini wewe husikilizi?
Au kukulilia, “Udhalimu!”
Lakini hutaki kuokoa?
3 1:3Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma?
Kwa nini unavumilia makosa?
Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu;
kuna mabishano na mapambano kwa wingi.
4 1:4Kwa hiyo sheria imepotoshwa,
nayo haki haipo kabisa.
Waovu wanawazunguka wenye haki,
kwa hiyo haki imepotoshwa.
Jibu La
Bwana
5 1:5“Yatazame mataifa,
uangalie na ushangae kabisa.
Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu
ambacho hungeamini,
hata kama ungeambiwa.
6 1:6Nitawainua Wakaldayo,
watu hao wakatili na wenye haraka,
ambao hupita dunia yote
kuteka mahali pa kuishi pasipo pao wenyewe.
7 1:7Ni watu wanoogopwa na wanaotisha;
wenyewe ndio sheria yao,
na huinua heshima yao wenyewe.
8 1:8Farasi wao ni wepesi kuliko chui,
na wakali kuliko mbwa mwitu wakati wa machweo.
Askari wapanda farasi wao huenda mbio;
waendesha farasi wao wanatoka mbali.
Wanaruka kasi kama tai ili kurarua;
9 1:9wote wanakuja tayari kwa fujo.
Makundi yao ya wajeuri yanasonga mbele
kama upepo wa jangwani,
na kukusanya wafungwa
kama mchanga.
10 1:10Wanawabeza wafalme,
na kuwadhihaki watawala.
Wanaicheka miji yote iliyozungushiwa maboma;
wanafanya malundo ya udongo na kuiteka hiyo miji.
11 1:11Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele:
watu wenye hatia, ambao nguvu zao ndio mungu wao.”
Lalamiko La Pili La Habakuki
12 1:12Ee
Bwana, je, wewe sio wa tangu milele?
Mungu wangu, Uliye Mtakatifu wangu, hatutakufa.
Ee
Bwana, umewachagua wao ili watekeleze hukumu;
Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.
13 1:13Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu,
wala huwezi kuvumilia makosa.
Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu?
Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu
wanawameza wale wenye haki
kuliko wao wenyewe?
14 1:14Umewafanya watu kama samaki baharini,
kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.
15 1:15Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana,
anawakamata katika wavu wake,
anawakusanya katika juya lake;
kwa hiyo anashangilia na anafurahi.
16 1:16Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake,
na kuchoma uvumba kwa juya lake,
kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe,
na anafurahia chakula kizuri.
17 1:17Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake,
akiangamiza mataifa bila huruma?
21 2:1Nitasimama katika zamu yangu,
na kujiweka mwenyewe juu ya maboma;
nitatazama nione atakaloniambia,
na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.
Jibu La
Bwana
2 2:2Kisha
Bwana akajibu:
“Andika ufunuo huu,
na ukaufanye wazi juu ya vibao,
ili mpiga mbiu akimbie nao.
3 2:3Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika;
unazungumzia mambo ya mwisho,
na kamwe hautakosea.
Iwapo utakawia, wewe usubiri;
kwa hakika utakuja na hautachelewa.
4 2:4“Tazama, amejaa majivuno;
anavyovitamani si vya unyofu:
lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:
5 2:5hakika mvinyo humsaliti;
ni mwenye kiburi na hana amani.
Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu
na kama kifo kamwe hatosheki;
anajikusanyia mataifa yote
na kuchukua watu wote mateka.
6 2:6“Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema,
“ ‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa
na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu!
Ataendelea hivi kwa muda gani?’
7 2:7Je, wadai wako hawatainuka ghafula?
Je, hawataamka na kukufanya utetemeke?
Kisha utakuwa mhanga kwao.
8 2:8Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi,
watu waliobaki watakuteka nyara wewe.
Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu;
umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.
9 2:9“Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu,
awekaye kiota chake juu,
ili kukimbia makucha ya uharibifu!
10 2:10Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi,
ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.
11 2:11Mawe ya kuta yatapiga kelele,
na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.
12 2:12“Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga
damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!
13 2:13Je,
Bwana Mwenye Nguvu Zote hakuonyesha
kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto,
na kwamba mataifa
yanajichosha bure?
14 2:14Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa
Bwana,
kama maji yaifunikavyo bahari.
15 2:15“Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo,
akiimimina kutoka kwenye kiriba
cha mvinyo mpaka wamelewa,
ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.
16 2:16Utajazwa na aibu badala ya utukufu.
Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue!
Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume wa
Bwana kinakujia,
na aibu itafunika utukufu wako.
17 2:17Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika,
na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha.
Kwa sababu umemwaga damu ya mtu;
umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.
18 2:18“Sanamu ina thamani gani,
kwani mwanadamu ndiye alichonga?
Ama kinyago kinachofundisha uongo?
Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza
hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe;
hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.
19 2:19Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’
Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’
Je, linaweza kuongoza?
Limefunikwa kwa dhahabu na fedha;
hakuna pumzi ndani yake.
20 2:20Lakini
Bwana yuko katika Hekalu lake takatifu;
dunia yote na inyamaze mbele yake.”
3Maombi Ya Habakuki
1 3:1Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
3:1
Ni kifaa cha uimbaji chenye nyuzi; pia maombi kutumia kifaa hiki.
2 3:2
Bwana, nimezisikia sifa zako;
nami naogopa kwa matendo yako, Ee
Bwana.
Fufua kazi yako katikati ya miaka,
katikati ya miaka tangaza habari yako;
katika ghadhabu kumbuka rehema.
3 3:3Mungu alitoka Temani,
yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani.
Utukufu wake ulifunika mbingu,
na sifa zake zikaifunika dunia.
4 3:4Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo;
mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake,
ambako nguvu zake zilifichwa.
5 3:5Tauni ilimtangulia;
maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
6 3:6Alisimama, akaitikisa dunia;
alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke.
Milima ya zamani iligeuka mavumbi
na vilima vilivyozeeka vikaanguka.
Njia zake ni za milele.
7 3:7Niliona watu wa Kushani katika dhiki,
na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
8 3:8Ee
Bwana, uliikasirikia mito?
Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito?
Je, ulighadhibikia bahari
ulipoendesha farasi wako
na magari yako ya ushindi?
9 3:9Uliufunua upinde wako
na kuita mishale mingi.
Uliigawa dunia kwa mito;
10 3:10milima ilikuona ikatetemeka.
Mafuriko ya maji yakapita huko;
vilindi vilinguruma
na kuinua mawimbi yake juu.
11 3:11Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni
katika mngʼao wa mishale yako inayoruka,
na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
12 3:12Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia,
na katika hasira ulikanyaga mataifa.
13 3:13Ulikuja kuwaokoa watu wako,
kumwokoa uliyemtia mafuta.
Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu,
ukamvua toka kichwani hadi wayo.
14 3:14Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake
wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya,
wakifurahi kama walio karibu kutafuna
wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
15 3:15Ulikanyaga bahari kwa farasi wako,
ukisukasuka maji makuu.
16 3:16Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu,
midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti;
uchakavu ukanyemelea mifupa yangu,
na miguu yangu ikatetemeka.
Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa
kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
17 3:17Ingawa mtini hauchanui maua
na hakuna zabibu juu ya mizabibu,
ingawaje mzeituni hauzai,
na hata mashamba hayatoi chakula,
iwapo hakuna kondoo katika banda,
wala ngʼombe katika zizi,
18 3:18hata hivyo nitashangilia katika
Bwana,
nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
19 3:19
Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu;
huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala,
huniwezesha kupita juu ya vilima.
Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.