Hosea
1Hosea1 1:1Neno la
Bwana lililomjia Hosea mwana wa Beeri wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na wakati wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi, mfalme wa Israeli.
Mke Wa Hosea Na Watoto
2 1:2Wakati
Bwana alipoanza kuzungumza kupitia Hosea,
Bwana alimwambia, “Nenda ukajitwalie mwanamke wa uzinzi na watoto wa uzinzi, kwa sababu nchi ina hatia ya uzinzi wa kupindukia kwa kumwacha
Bwana.”
3 1:3Kwa hiyo alimwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba na kumzalia Hosea mwana.
4 1:4Kisha
Bwana akamwambia Hosea, “Mwite Yezreeli,
1:4
Yezreeli maana yake Mungu hupanda. kwa kuwa kitambo kidogo nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa ajili ya mauaji ya kule Yezreeli, nami nitaukomesha ufalme wa Israeli.
5 1:5Katika siku ile nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde la Yezreeli.”
6 1:6Gomeri akachukua tena mimba akamzaa binti. Kisha
Bwana akamwambia Hosea, “Mwite Lo-Ruhama,
1:6
Lo-Ruhama maana yake Sio mpenzi wangu. kwa maana sitaonyesha tena upendo kwa nyumba ya Israeli, kwamba nisije kabisa nikawasamehe.
7 1:7Hata hivyo nitaonyesha upendo kwa nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa si kwa upinde, upanga au vita, wala kwa farasi na wapanda farasi, bali kwa njia ya
Bwana Mungu wao.”
8 1:8Baada ya Gomeri kumwachisha Lo-Ruhama kunyonya, Gomeri alipata mwana mwingine.
9 1:9Kisha
Bwana akasema, “Mwite Lo-Ami
1:9
Lo-Ami maana yake Sio watu wangu. kwa maana ninyi si watu wangu, nami si Mungu wenu.
10 1:10“Hata hivyo Waisraeli watakuwa kama mchanga kando ya bahari, ambao hauwezi kupimika wala kuhesabiwa. Mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’
11 1:11Watu wa Yuda na watu wa Israeli wataunganishwa tena, nao watamchagua kiongozi mmoja nao watakwea watoke katika nchi, kwa kuwa siku ya Yezreeli itakuwa kuu sana.
21 2:1“Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
Israeli Aadhibiwa Na Kurudishwa
2 2:2“Mkemeeni mama yenu, mkemeeni,
kwa maana yeye si mke wangu,
nami si mume wake.
Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake
na uzinzi kati ya matiti yake.
3 2:3Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi
na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa.
Nitamfanya kama jangwa,
nitamgeuza awe nchi ya kiu,
nami nitamuua kwa kiu.
4 2:4Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake,
kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
5 2:5Mama yao amekosa uaminifu
na amewachukua mimba katika aibu.
Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu,
ambao hunipa chakula changu
na maji yangu,
sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu
na kinywaji changu.’
6 2:6Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake
kwa vichaka vya miiba,
nitamjengea ukuta ili kwamba
asiweze kutoka.
7 2:7Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata;
atawatafuta lakini hatawapata.
Kisha atasema,
‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza,
kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi
kuliko sasa.’
8 2:8Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye
niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta,
niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia
kwa kumtumikia Baali.
9 2:9“Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa
na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari.
Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu
iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
10 2:10Basi sasa nitaufunua ufisadi wake
mbele ya wapenzi wake;
hakuna yeyote atakayemtoa
mikononi mwangu.
11 2:11Nitakomesha furaha na macheko yake yote:
sikukuu zake za mwaka,
sikukuu za Miandamo ya Mwezi,
siku zake za Sabato,
sikukuu zake zote zilizoamriwa.
12 2:12Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake,
ambayo alisema yalikuwa malipo yake
kutoka kwa wapenzi wake;
nitaifanya kuwa kichaka,
nao wanyama pori wataila.
13 2:13Nitamwadhibu kwa ajili ya siku
alizowafukizia uvumba Mabaali;
alipojipamba kwa pete
na kwa vito vya thamani,
na kuwaendea wapenzi wake,
lakini mimi alinisahau,”
asema
Bwana.
14 2:14“Kwa hiyo sasa nitamshawishi;
nitamwongoza hadi jangwani
na kuzungumza naye kwa upole.
15 2:15Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu,
nami nitalifanya Bonde la Akori
2:15
Akori maana yake ni Taabu.
mlango wa matumaini.
Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake,
kama siku zile alizotoka Misri.
16 2:16“Katika siku ile,” asema
Bwana,
“utaniita mimi ‘Mume wangu’;
hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
17 2:17Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake,
wala hataomba tena kwa majina yao.
18 2:18Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao
na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani,
na viumbe vile vitambaavyo ardhini.
Upinde, upanga na vita,
nitaondolea mbali katika nchi,
ili kwamba wote waweze kukaa salama.
19 2:19Nitakuposa uwe wangu milele;
nitakuposa kwa uadilifu na haki,
kwa upendo na huruma.
20 2:20Nitakuposa kwa uaminifu,
nawe utamkubali
Bwana.
21 2:21“Katika siku ile nitajibu,”
asema
Bwana,
“nitajibu kwa anga,
nazo anga zitajibu kwa nchi;
22 2:22nayo nchi itajibu kwa nafaka,
divai mpya na mafuta,
navyo vitajibu kwa Yezreeli.
23 2:23Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe;
nami nitaonyesha pendo langu kwake
yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.
2:23
Kiebrania ni Lo-Ruhama.’
Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’
2:23
Kiebrania ni Lo-Ami.
‘Ninyi ni watu wangu’;
nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’ ”
3Upatanisho Wa Hosea Na Mkewe
1 3:1
Bwana akaniambia, “Nenda, ukaonyeshe upendo wako kwa mke wako tena, ingawa amependwa na mwingine naye ni mzinzi. Mpende kama
Bwana apendavyo Waisraeli, ingawa wanageukia miungu mingine na kupenda mikate mitamu ya zabibu kavu iliyowekwa wakfu.”
2 3:2Basi nilimnunua huyo mwanamke kwa shekeli kumi na tano
3:2
Shekeli 15 za fedha ni sawa na gramu 170. za fedha, pia kwa kiasi kama cha homeri moja na nusu
3:2
Homeri moja na nusu ni kama lita 330. ya shayiri.
3 3:3Kisha nilimwambia, “Utaishi nami kwa siku nyingi, hupaswi kuwa kahaba au kuwa na uhusiano wa karibu na mtu yeyote, nami nitaishi na wewe.”
4 3:4Kwa maana Waisraeli wataishi siku nyingi bila kuwa na mfalme wala mkuu, bila kuwa na dhabihu wala mawe matakatifu, bila kisibau wala sanamu.
5 3:5Baadaye Waisraeli watarudi na kumtafuta
Bwana Mungu wao na Daudi mfalme wao. Watakuja wakitetemeka kwa
Bwana na kwa baraka zake katika siku za mwisho.
4Shtaka Dhidi Ya Israeli
1 4:1Sikieni neno la
Bwana, enyi Waisraeli,
kwa sababu
Bwana analo shtaka
dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:
“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,
hakuna kumjua Mungu katika nchi.
2 4:2Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,
wizi na uzinzi,
bila kuwa na mipaka,
nao umwagaji damu mmoja
baada ya mwingine.
3 4:3Kwa sababu hii nchi huomboleza,
wote waishio ndani mwake wanadhoofika,
wanyama wa kondeni, ndege wa angani
na samaki wa baharini wanakufa.
4 4:4“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,
mtu yeyote na asimlaumu mwenzake,
kwa maana watu wako ni kama wale
waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
5 4:5Unajikwaa usiku na mchana,
nao manabii hujikwaa pamoja nawe.
Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
6 4:6watu wangu wanaangamizwa
kwa kukosa maarifa,
“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,
mimi nami nitakukataa wewe
usiwe kuhani kwangu mimi;
kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako
mimi nami sitawajali watoto wako.
7 4:7Kadiri makuhani walivyoongezeka,
ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,
walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
8 4:8Hujilisha dhambi za watu wangu
na kupendezwa na uovu wao.
9 4:9Hata itakuwa: Kama walivyo watu,
ndivyo walivyo makuhani.
Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao
na kuwalipa kwa matendo yao.
10 4:10“Watakula lakini hawatashiba;
watajiingiza katika ukahaba
lakini hawataongezeka,
kwa sababu wamemwacha
Bwana
na kujiingiza wenyewe
11 4:11katika ukahaba,
divai ya zamani na divai mpya,
ambavyo huondoa ufahamu
12 4:12wa watu wangu.
Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti
nao hujibiwa na fimbo ya mti.
Roho ya ukahaba imewapotosha,
hawana uaminifu kwa Mungu wao.
13 4:13Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima
na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,
chini ya mialoni, milibua na miela,
ambako kuna vivuli vizuri.
Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba
na wake za wana wenu uzinzi.
14 4:14“Sitawaadhibu binti zenu wakati
wanapogeukia ukahaba,
wala wake za wana wenu
wanapofanya uzinzi,
kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya
na kutambikia pamoja na makahaba
wa mahali pa kuabudia miungu:
watu wasiokuwa na ufahamu
wataangamia!
15 4:15“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli,
Yuda naye asije akawa na hatia.
“Usiende Gilgali,
usipande kwenda Beth-Aveni
4:15
Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.
Wala usiape,
‘Hakika kama
Bwana aishivyo!’
16 4:16Waisraeli ni wakaidi,
kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi.
Ni jinsi gani basi
Bwana anaweza kuwachunga
kama wana-kondoo
katika shamba la majani?
17 4:17Efraimu amejiunga na sanamu,
ondokana naye!
18 4:18Hata wakati wamemaliza vileo vyao
wanaendelea na ukahaba wao,
watawala wao hupenda sana
njia za aibu.
19 4:19Kisulisuli kitawafagilia mbali
na dhabihu zao zitawaletea aibu.
5Hukumu Dhidi Ya Israeli
1 5:1“Sikieni hili, enyi makuhani!
Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli!
Sikieni, ee nyumba ya mfalme!
Hukumu hii ni dhidi yenu:
Mmekuwa mtego huko Mispa,
wavu uliotandwa juu ya Tabori.
2 5:2Waasi wamezidisha sana mauaji.
Mimi nitawatiisha wote.
3 5:3Ninajua yote kuhusu Efraimu,
Israeli hukufichika kwangu.
Efraimu, sasa umegeukia ukahaba,
Israeli amenajisika.
4 5:4“Matendo yao hayawaachii
kurudi kwa Mungu wao.
Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao,
hawamkubali
Bwana.
5 5:5Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao;
Waisraeli, hata Efraimu,
wanajikwaa katika dhambi zao;
pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
6 5:6Wakati wanapokwenda na makundi yao
ya kondoo na ngʼombe
kumtafuta
Bwana,
hawatampata;
yeye amejiondoa kutoka kwao.
7 5:7Wao si waaminifu kwa
Bwana;
wamezaa watoto haramu.
Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi
zitawaangamiza wao
pamoja na mashamba yao.
8 5:8“Pigeni tarumbeta huko Gibea,
baragumu huko Rama.
Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni,
5:8
Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.
ongoza, ee Benyamini.
9 5:9Efraimu ataachwa ukiwa
katika siku ya kuadhibiwa.
Miongoni mwa makabila ya Israeli
ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
10 5:10Viongozi wa Yuda ni kama wale
wanaosogeza mawe ya mpaka.
Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao
kama mafuriko ya maji.
11 5:11Efraimu ameonewa,
amekanyagwa katika hukumu
kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
12 5:12Mimi ni kama nondo kwa Efraimu,
na kama uozo kwa watu wa Yuda.
13 5:13“Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake,
naye Yuda vidonda vyake,
ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru,
na kuomba msaada kwa mfalme mkuu.
Lakini hawezi kukuponya,
wala hawezi kukuponya vidonda vyako.
14 5:14Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu,
kama simba mkubwa kwa Yuda.
Nitawararua vipande vipande na kuondoka;
nitawachukua mbali,
na hakuna wa kuwaokoa.
15 5:15Kisha nitarudi mahali pangu
mpaka watakapokubali kosa lao.
Nao watautafuta uso wangu;
katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
6Israeli Asiye Na Toba
1 6:1“Njooni, tumrudie
Bwana.
Ameturarua vipande vipande
lakini atatuponya;
ametujeruhi lakini
atatufunga majeraha yetu.
2 6:2Baada ya siku mbili atatufufua;
katika siku ya tatu atatuinua,
ili tuweze kuishi mbele zake.
3 6:3Tumkubali
Bwana,
tukaze kumkubali yeye.
Kutokea kwake ni hakika kama vile
kuchomoza kwa jua;
atatujia kama mvua za masika,
kama vile mvua za vuli
ziinyweshavyo nchi.”
4 6:4“Nifanye nini nawe, Efraimu?
Nifanye nini nawe, Yuda?
Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi,
kama umande wa alfajiri utowekao.
5 6:5Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande
kwa kutumia manabii wangu;
nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu,
hukumu zangu zinawaka
kama umeme juu yenu.
6 6:6Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu,
kumkubali Mungu zaidi
kuliko sadaka za kuteketezwa.
7 6:7Wamevunja Agano kama Adamu:
huko hawakuwa waaminifu kwangu.
8 6:8Gileadi ni mji wenye watu waovu,
umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
9 6:9Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu,
ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo;
wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu,
wakifanya uhalifu wa aibu.
10 6:10Nimeona jambo la kutisha
katika nyumba ya Israeli.
Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba
na Israeli amenajisika.
11 6:11“Pia kwa ajili yako, Yuda,
mavuno yameamriwa.
“Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,
71 7:1kila mara nilipotaka kumponya Israeli,
dhambi za Efraimu zinafichuliwa
na maovu ya Samaria yanafunuliwa.
Wanafanya udanganyifu,
wevi huvunja nyumba,
maharamia hunyangʼanya barabarani,
2 7:2lakini hawafahamu kwamba
ninakumbuka matendo yao yote mabaya.
Dhambi zao zimewameza,
ziko mbele zangu siku zote.
3 7:3“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao,
wakuu wao kwa uongo wao.
4 7:4Wote ni wazinzi,
wanawaka kama tanuru
ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea
kuanzia kukanda unga
hadi umekwisha kuumuka.
5 7:5Katika sikukuu ya mfalme wetu
wakuu wanawaka kwa mvinyo,
naye anawaunga mkono wenye mizaha.
6 7:6Mioyo yao ni kama tanuru,
wanamwendea kwa hila.
Hasira yao inafoka moshi usiku kucha,
wakati wa asubuhi inalipuka
kama miali ya moto.
7 7:7Wote ni moto kama tanuru;
wanawaangamiza watawala wao.
Wafalme wake wote wanaanguka,
wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
8 7:8“Efraimu anajichanganya na mataifa;
Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
9 7:9Wageni wananyonya nguvu zake,
lakini hafahamu hilo.
Nywele zake zina mvi hapa na pale,
lakini hana habari.
10 7:10Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake,
lakini pamoja na haya yote
harudi kwa
Bwana Mungu wake
wala kumtafuta.
11 7:11“Efraimu ni kama hua,
hudanganywa kwa urahisi na hana akili:
mara anaita Misri,
mara anageukia Ashuru.
12 7:12Wakati watakapokwenda,
nitatupa wavu wangu juu yao;
nitawavuta chini waanguke
kama ndege wa angani.
Nitakaposikia wakikusanyika pamoja,
nitawanasa.
13 7:13Ole wao, kwa sababu
wamepotoka kutoka kwangu!
Maangamizi ni yao
kwa sababu wameniasi!
Ninatamani kuwakomboa,
lakini wanasema uongo dhidi yangu.
14 7:14Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao,
bali wanaomboleza vitandani mwao.
Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya,
lakini hugeukia mbali nami.
15 7:15Niliwafundisha na kuwatia nguvu,
lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 7:16Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana,
wako kama upinde wenye kasoro.
Viongozi wao wataanguka kwa upanga
kwa sababu ya maneno yao ya jeuri.
Kwa ajili ya hili watadhihakiwa
katika nchi ya Misri.
8Israeli Kuvuna Kisulisuli
1 8:1“Wekeni tarumbeta midomoni mwenu!
Tai yuko juu ya nyumba ya
Bwana
kwa sababu watu wamevunja Agano langu,
wameasi dhidi ya sheria yangu.
2 8:2Israeli ananililia,
‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
3 8:3Lakini Israeli amekataa lile lililo jema,
adui atamfuatia.
4 8:4Wanaweka wafalme bila idhini yangu,
wamechagua wakuu bila kibali changu.
Kwa fedha zao na dhahabu
wamejitengenezea sanamu kwa ajili
ya maangamizi yao wenyewe.
5 8:5Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama!
Hasira yangu inawaka dhidi yao.
Watakuwa najisi mpaka lini?
6 8:6Zimetoka katika Israeli!
Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu.
Atavunjwa vipande vipande,
yule ndama wa Samaria.
7 8:7“Wanapanda upepo
na kuvuna upepo wa kisulisuli.
Bua halina suke,
halitatoa unga.
Kama lingetoa nafaka,
wageni wangeila yote.
8 8:8Israeli amemezwa;
sasa yupo miongoni mwa mataifa
kama kitu kisicho na thamani.
9 8:9Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru
kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake.
Efraimu amejiuza mwenyewe
kwa wapenzi.
10 8:10Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa,
sasa nitawakusanya pamoja.
Wataanza kudhoofika chini ya uonevu
wa mfalme mwenye nguvu.
11 8:11“Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi
kwa ajili ya sadaka za dhambi,
hizi zimekuwa madhabahu
za kufanyia dhambi.
12 8:12Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi
kuhusu sheria yangu,
lakini wameziangalia
kama kitu cha kigeni.
13 8:13Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi
nao wanakula hiyo nyama,
lakini
Bwana hapendezwi nao.
Sasa ataukumbuka uovu wao
na kuadhibu dhambi zao:
Watarudi Misri.
14 8:14Israeli amemsahau Muumba wake
na kujenga majumba ya kifalme,
Yuda amejengea miji mingi ngome.
Lakini nitatuma moto kwenye miji yao
utakaoteketeza ngome zao.”
9Adhabu Kwa Israeli
1 9:1Usifurahie, ee Israeli;
usishangilie kama mataifa mengine.
Kwa kuwa hukuwa
mwaminifu kwa Mungu wako;
umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu
ya kupuria nafaka.
2 9:2Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai
havitalisha watu,
divai mpya itawapungukia.
3 9:3Hawataishi katika nchi ya
Bwana,
Efraimu atarudi Misri
na atakula chakula
kilicho najisi huko Ashuru.
4 9:4Hawatammiminia
Bwana sadaka ya divai
wala dhabihu zao hazitampendeza.
Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao
kama mkate wa waombolezaji;
nao wote wazilao watakuwa najisi.
Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe;
kisije katika Hekalu la
Bwana.
5 9:5Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa,
katika siku za sikukuu za
Bwana?
6 9:6Hata ikiwa wataokoka maangamizi,
Misri atawakusanya,
nayo Memfisi
9:6
Memfisi kwa Kiebrania ni Nofu. itawazika.
Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma,
nayo miiba itafunika mahema yao.
7 9:7Siku za adhabu zinakuja,
siku za malipo zimewadia.
Israeli na afahamu hili.
Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana
na uadui wenu ni mkubwa sana,
nabii anadhaniwa ni mpumbavu,
mtu aliyeongozwa na Mungu
anaonekana mwendawazimu.
8 9:8Nabii, pamoja na Mungu wangu,
ndiye mlinzi juu ya Efraimu,
hata hivyo mitego inamngojea
katika mapito yake yote,
na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
9 9:9Wamezama sana katika rushwa,
kama katika siku za Gibea.
Mungu atakumbuka uovu wao
na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
10 9:10“Nilipompata Israeli, ilikuwa kama
kupata zabibu jangwani;
nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona
matunda ya kwanza katika mtini.
Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu
kwa ile sanamu ya aibu,
nao wakawa najisi
kama kitu kile walichokipenda.
11 9:11Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege:
hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba,
hakuna kutunga mimba.
12 9:12Hata wakilea watoto,
nitamuua kila mmoja.
Ole wao
nitakapowapiga kisogo!
13 9:13Nimemwona Efraimu, kama Tiro,
aliyeoteshwa mahali pazuri.
Lakini Efraimu wataleta
watoto wao kwa mchinjaji.”
14 9:14Wape, Ee
Bwana,
je, utawapa nini?
Wape matumbo ya kuharibu mimba
na matiti yaliyokauka.
15 9:15“Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali,
niliwachukia huko.
Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi,
nitawafukuza katika nyumba yangu.
Sitawapenda tena,
viongozi wao wote ni waasi.
16 9:16Efraimu ameharibiwa,
mzizi wao umenyauka,
hawazai tunda.
Hata kama watazaa watoto,
nitawachinja watoto wao
waliotunzwa vizuri.”
17 9:17Mungu wangu atawakataa
kwa sababu hawakumtii;
watakuwa watu wa kutangatanga
miongoni mwa mataifa.
101 10:1Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana,
alijizalia matunda mwenyewe.
Kadiri matunda yake yalivyoongezeka,
alijenga madhabahu zaidi;
kadiri nchi yake ilivyostawi,
alipamba mawe yake ya ibada.
2 10:2Moyo wao ni mdanganyifu,
nao sasa lazima wachukue hatia yao.
Bwana atabomoa madhabahu zao
na kuharibu mawe yao ya ibada.
3 10:3Kisha watasema, “Hatuna mfalme
kwa sababu hatukumheshimu
Bwana.
Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme,
angeweza kutufanyia nini?”
4 10:4Wanaweka ahadi nyingi,
huapa viapo vya uongo
wanapofanya mapatano;
kwa hiyo mashtaka huchipuka
kama magugu ya sumu
katika shamba lililolimwa.
5 10:5Watu wanaoishi Samaria huogopa
kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni.
10:5
Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.
Watu wake wataiombolezea,
vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu,
wale waliokuwa wamefurahia fahari yake,
kwa sababu itaondolewa kutoka kwao
kwenda uhamishoni.
6 10:6Itachukuliwa kwenda Ashuru
kama ushuru kwa mfalme mkuu.
Efraimu atafedheheshwa;
Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
7 10:7Samaria na mfalme wake wataelea
kama kijiti juu ya uso wa maji.
8 10:8Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu
10:8
Yaani
Aveni
kwa Kiebrania, kumaanisha
Beth-Aveni, jina lingine la Betheli kwa dhihaka. pataharibiwa:
ndiyo dhambi ya Israeli.
Miiba na mibaruti itaota
na kufunika madhabahu zao.
Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!”
na vilima, “Tuangukieni!”
9 10:9“Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli,
huko ndiko mlikobaki.
Je, vita havikuwapata
watenda mabaya huko Gibea?
10 10:10Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu;
mataifa yatakusanywa dhidi yao
ili kuwaweka katika vifungo
kwa ajili ya dhambi zao mbili.
11 10:11Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa
ambaye hupenda kupura,
hivyo nitamfunga nira
juu ya shingo yake nzuri.
Nitamwendesha Efraimu,
Yuda lazima alime,
naye Yakobo lazima avunjavunje
mabonge ya udongo.
12 10:12Jipandieni wenyewe haki,
vuneni matunda ya upendo usio na kikomo,
vunjeni ardhi yenu isiyolimwa;
kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta
Bwana,
mpaka atakapokuja
na kuwanyeshea juu yenu haki.
13 10:13Lakini mmepanda uovu,
mkavuna ubaya,
mmekula tunda la udanganyifu.
Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe
na wingi wa mashujaa wenu,
14 10:14mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako,
ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa:
kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita,
wakati mama pamoja na watoto wao
walipotupwa kwa nguvu ardhini.
15 10:15Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli,
kwa sababu uovu wako ni mkuu.
Siku ile itakapopambazuka,
mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
11Upendo Wa Mungu Kwa Israeli
1 11:1“Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda,
nilimwita mwanangu kutoka Misri.
2 11:2Lakini kadiri nilivyomwita Israeli,
ndivyo walivyokwenda mbali nami.
Walitoa dhabihu kwa Mabaali
na kufukiza uvumba kwa vinyago.
3 11:3Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea,
nikiwashika mikono;
lakini hawakutambua
kuwa ni mimi niliyewaponya.
4 11:4Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu,
kwa vifungo vya upendo;
niliondoa nira shingoni mwao
nami nikainama kuwalisha.
5 11:5“Je, hawatarudi Misri,
nayo Ashuru haitawatawala
kwa sababu wamekataa kutubu?
6 11:6Panga zitametameta katika miji yao,
zitaharibu makomeo ya malango yao
na kukomesha mipango yao.
7 11:7Watu wangu wamedhamiria kuniacha.
Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana,
kwa vyovyote hatawainua.
8 11:8“Efraimu, ninawezaje kukuacha?
Ee Israeli, ninawezaje kukutoa?
Nitawezaje kukutendea kama Adma?
Nitawezaje kukufanya kama Seboimu?
Moyo wangu umegeuka ndani yangu,
huruma zangu zote zimeamshwa.
9 11:9Sitatimiza hasira yangu kali,
wala sitageuka na kumharibu Efraimu.
Kwa kuwa mimi ndimi Mungu,
wala si mwanadamu,
Aliye Mtakatifu miongoni mwenu.
Sitakuja kwa ghadhabu.
10 11:10Watamfuata
Bwana;
atanguruma kama simba.
Wakati angurumapo,
watoto wake watakuja wakitetemeka
kutoka magharibi.
11 11:11Watakuja wakitetemeka
kama ndege wakitoka Misri,
kama hua wakitoka Ashuru.
Nitawakalisha katika nyumba zao,”
asema
Bwana.
Dhambi Ya Israeli
12 11:12Efraimu amenizunguka kwa uongo,
nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.
Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu,
hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.
121 12:1Efraimu anajilisha upepo;
hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima
na kuzidisha uongo na jeuri.
Anafanya mkataba na Ashuru
na kutuma mafuta ya zeituni Misri.
2 12:2
Bwana analo shtaka dhidi ya Yuda,
atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake
na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake.
3 12:3Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake;
kama mwanadamu, alishindana na Mungu.
4 12:4Alishindana na malaika na kumshinda;
alilia na kuomba upendeleo wake.
Alimkuta huko Betheli
na kuzungumza naye huko:
5 12:5
Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote,
Bwana ndilo jina lake!
6 12:6Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako;
dumisha upendo na haki,
nawe umngojee Mungu wako siku zote.
7 12:7Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu;
hupenda kupunja.
8 12:8Efraimu hujisifu akisema,
“Mimi ni tajiri sana; nimetajirika.
Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu
uovu wowote au dhambi.”
9 12:9“Mimi ndimi
Bwana Mungu wenu
niliyewaleta kutoka Misri;
nitawafanya mkae tena kwenye mahema,
kama vile katika siku
za sikukuu zenu zilizoamriwa.
10 12:10Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi
na kusema mifano kupitia wao.”
11 12:11Je, Gileadi si mwovu?
Watu wake hawafai kitu!
Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali?
Madhabahu zao zitakuwa
kama malundo ya mawe
katika shamba lililolimwa.
12 12:12Yakobo alikimbilia katika nchi ya Aramu;
Israeli alitumika ili apate mke,
ili aweze kulipa kwa ajili yake alichunga kondoo.
13 12:13
Bwana alimtumia nabii
kumpandisha Israeli kutoka Misri,
kwa njia ya nabii alimtunza.
14 12:14Lakini Efraimu amemchochea sana hasira;
Bwana wake ataleta juu yake
hatia yake ya kumwaga damu naye atamlipiza
kwa ajili ya dharau yake.
13Hasira Ya
Bwana Dhidi Ya Israeli
1 13:1Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka,
alikuwa ametukuzwa katika Israeli.
Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali
naye akafa.
2 13:2Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi;
wanajitengenezea sanamu
kutokana na fedha yao,
vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari,
vyote kazi ya fundi stadi.
Inasemekana kuhusu hawa watu,
“Hutoa dhabihu za binadamu
na kubusu sanamu za ndama.”
3 13:3Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,
kama umande wa alfajiri utowekao,
kama makapi yapeperushwayo
kutoka sakafu ya kupuria nafaka,
kama moshi utorokao kupitia dirishani.
4 13:4“Bali mimi ndimi
Bwana Mungu wenu,
niliyewaleta ninyi toka Misri.
Msimkubali Mungu mwingine ila mimi,
hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
5 13:5Niliwatunza huko jangwani,
katika nchi yenye joto liunguzalo.
6 13:6Nilipowalisha, walishiba,
waliposhiba, wakajivuna,
kisha wakanisahau mimi.
7 13:7Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba,
kama chui nitawavizia kando ya njia.
8 13:8Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,
nitawashambulia na kurarua vifua vyenu.
Kama simba nitawala;
mnyama pori atawararua vipande vipande.
9 13:9“Ee Israeli, umeangamizwa,
kwa sababu wewe u kinyume nami,
kinyume na msaidizi wako.
10 13:10Yuko wapi mfalme wako,
ili apate kukuokoa?
Wako wapi watawala wako katika miji yako yote
ambao ulisema kuwahusu,
‘Nipe mfalme na wakuu’?
11 13:11Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme
na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
12 13:12Kosa la Efraimu limehifadhiwa,
dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
13 13:13Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia,
lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima;
wakati utakapowadia hatatoka
katika tumbo la mama yake.
14 13:14“Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi,
nitawakomboa kutoka mautini.
Yako wapi, ee mauti, mateso yako?
Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako?
“Sitakuwa na huruma,
15 13:15hata ingawa Efraimu atastawi
miongoni mwa ndugu zake.
Upepo wa mashariki kutoka kwa
Bwana utakuja,
ukivuma kutoka jangwani,
chemchemi yake haitatoa maji
na kisima chake kitakauka.
Ghala lake litatekwa
hazina zake zote.
16 13:16Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao,
kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao.
Wataanguka kwa upanga;
watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini,
wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”
14Toba Iletayo Baraka
1 14:1Rudi, ee Israeli, kwa
Bwana Mungu wako.
Dhambi zako zimekuwa
ndilo anguko lako!
2 14:2Chukueni maneno pamoja nanyi,
mkamrudie
Bwana.
Mwambieni:
“Samehe dhambi zetu zote
na utupokee kwa neema,
ili tuweze kutoa matunda yetu
kama sadaka za mafahali.
3 14:3Ashuru hawezi kutuokoa,
hatutapanda farasi wa vita.
Kamwe hatutasema tena ‘Miungu yetu’
kwa kile ambacho mikono yetu wenyewe imetengeneza,
kwa kuwa kwako wewe yatima hupata huruma.”
4 14:4“Nitaponya ukaidi wao
na kuwapenda kwa hiari yangu,
kwa kuwa hasira yangu imeondoka kwao.
5 14:5Nitakuwa kama umande kwa Israeli;
atachanua kama yungiyungi.
Kama mwerezi wa Lebanoni
atashusha mizizi yake chini;
6 14:6matawi yake yatatanda.
Fahari yake itakuwa kama mti wa mzeituni,
harufu yake nzuri kama mwerezi wa Lebanoni.
7 14:7Watu wataishi tena kwenye kivuli chake.
Atastawi kama nafaka.
Atachanua kama mzabibu,
nao umaarufu wake utakuwa
kama divai itokayo Lebanoni.
8 14:8Ee Efraimu, nina shughuli gani tena na sanamu?
Nitamjibu na kumtunza.
Mimi ni kama msunobari wenye majani mabichi;
kuzaa kwako matunda kunatoka kwangu.”
9 14:9Ni nani mwenye hekima? Atayatambua mambo haya.
Ni nani mwenye ufahamu? Huyu atayaelewa.
Njia za
Bwana ni adili;
wenye haki huenda katika njia hizo,
lakini waasi watajikwaa ndani yake.