Maombolezo 1 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 1Maombolezo1 1:1Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa, mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu! Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane, ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa! Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo sasa amekuwa mtumwa. 2 1:2Kwa uchungu, hulia sana usiku, machozi yapo kwenye mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji. Rafiki zake wote wamemsaliti, wamekuwa adui zake. 3 1:3Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili, Yuda amekwenda uhamishoni. Anakaa miongoni mwa mataifa, hapati mahali pa kupumzika. Wote ambao wanamsaka wamemkamata katikati ya dhiki yake. 4 1:4Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza, kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja kwenye sikukuu zake zilizoamriwa. Malango yake yote yamekuwa ukiwa, makuhani wake wanalia kwa uchungu, wanawali wake wanahuzunika, naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu. 5 1:5Adui zake wamekuwa mabwana zake, watesi wake wana raha. Bwana amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi. Watoto wake wamekwenda uhamishoni, mateka mbele ya adui. 6 1:6Fahari yote imeondoka kutoka kwa Binti Sayuni. Wakuu wake wako kama ayala ambaye hapati malisho, katika udhaifu wamekimbia mbele ya anayewasaka. 7 1:7Katika siku za mateso yake na kutangatanga, Yerusalemu hukumbuka hazina zote ambazo zilikuwa zake siku za kale. Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui, hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia. Watesi wake walimtazama na kumcheka katika maangamizi yake. 8 1:8Yerusalemu ametenda dhambi sana kwa hiyo amekuwa najisi. Wote waliomheshimu wanamdharau, kwa maana wameuona uchi wake. Yeye mwenyewe anapiga kite na kugeukia mbali. 9 1:9Uchafu wake umegandamana na nguo zake; hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye. Anguko lake lilikuwa la kushangaza, hapakuwepo na yeyote wa kumfariji. “Tazama, Ee Bwana, teso langu, kwa maana adui ameshinda.” 10 1:10Adui ametia mikono juu ya hazina zake zote, aliona mataifa ya kipagani wakiingia mahali patakatifu pake, wale uliowakataza kuingia kwenye kusanyiko lako. 11 1:11Watu wake wote wanalia kwa uchungu watafutapo chakula; wanabadilisha hazina zao kwa chakula ili waweze kuendelea kuishi. “Tazama, Ee Bwana, ufikiri, kwa maana nimedharauliwa.” 12 1:12“Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando? Angalieni kote mwone. Je, kuna maumivu kama maumivu yangu yale yaliyotiwa juu yangu, yale Bwana aliyoyaleta juu yangu katika siku ya hasira yake kali? 13 1:13“Kutoka juu alipeleka moto, akaushusha katika mifupa yangu. Aliitandia wavu miguu yangu na akanirudisha nyuma. Akanifanya mkiwa, na mdhaifu mchana kutwa. 14 1:14“Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira, kwa mikono yake zilifumwa pamoja. Zimefika shingoni mwangu na Bwana ameziondoa nguvu zangu. Amenitia mikononi mwa wale ambao siwezi kushindana nao. 15 1:15“Bwana amewakataa wapiganaji wa vita wote walio kati yangu, ameagiza jeshi dhidi yangu kuwaponda vijana wangu wa kiume. Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga Bikira Binti Yuda. 16 1:16“Hii ndiyo sababu ninalia na macho yangu yanafurika machozi. Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji, hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu. Watoto wangu ni wakiwa kwa sababu adui ameshinda.” 17 1:17Sayuni ananyoosha mikono yake, lakini hakuna yeyote wa kumfariji. Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo kwamba majirani zake wawe adui zake; Yerusalemu umekuwa kitu najisi miongoni mwao. 18 1:18Bwana ni mwenye haki, hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake. Sikilizeni, enyi mataifa yote, tazameni maumivu yangu. Wavulana wangu na wasichana wangu wamekwenda uhamishoni. 19 1:19“Niliita washirika wangu lakini walinisaliti. Makuhani wangu na wazee wangu waliangamia mjini walipokuwa wakitafuta chakula ili waweze kuishi. 20 1:20“Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki! Nina maumivu makali ndani yangu, nami ninahangaika moyoni mwangu, kwa kuwa nimekuwa mwasi sana. Huko nje, upanga unaua watu, ndani, kipo kifo tu. 21 1:21“Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu, lakini hakuna yeyote wa kunifariji. Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu, wanafurahia lile ulilolitenda. Naomba uilete siku uliyoitangaza ili wawe kama mimi. 22 1:22“Uovu wao wote na uje mbele zako; uwashughulikie wao kama vile ulivyonishughulikia mimi kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi na moyo wangu umedhoofika.” 2 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 21 2:1Tazama jinsi Bwana alivyomfunika Binti Sayuni kwa wingu la hasira yake! Ameitupa chini fahari ya Israeli kutoka mbinguni mpaka duniani, hakukumbuka kiti chake cha kuwekea miguu katika siku ya hasira yake. 2 2:2Bila huruma Bwana ameyameza makao yote ya Yakobo; katika ghadhabu yake amebomoa ngome za Binti Yuda. Ameuangusha ufalme wake na wakuu wake chini kwa aibu. 3 2:3Katika hasira kali amevunja kila pembe 2:3 Pembe inawakilisha nguvu; pia 2:17. ya Israeli. Ameuondoa mkono wake wa kuume alipokaribia adui. Amemteketeza Yakobo kama moto uwakao ule uteketezao kila kitu kinachouzunguka. 4 2:4Ameupinda upinde wake kama adui, mkono wake wa kuume uko tayari. Kama vile adui amewachinja wote waliokuwa wanapendeza jicho, amemwaga ghadhabu yake kama moto juu ya hema la Binti Sayuni. 5 2:5Bwana ni kama adui; amemmeza Israeli. Amemeza majumba yake yote ya kifalme na kuangamiza ngome zake. Ameongeza huzuni na maombolezo kwa ajili ya Binti Yuda. 6 2:6Ameharibu maskani yake kama bustani, ameharibu mahali pake pa mkutano. Bwana amemfanya Sayuni kusahau sikukuu zake zilizoamriwa na Sabato zake; katika hasira yake kali amewadharau mfalme na kuhani. 7 2:7Bwana amekataa madhabahu yake na kuacha mahali patakatifu pake. Amemkabidhi adui kuta za majumba yake ya kifalme; wamepiga kelele katika nyumba ya Bwana kama katika siku ya sikukuu iliyoamriwa. 8 2:8 Bwana alikusudia kuangusha ukuta uliomzunguka Binti Sayuni. Ameinyoosha kamba ya kupimia na hakuuzuia mkono wake usiangamize. Alifanya maboma na kuta ziomboleze, vyote vikaharibika pamoja. 9 2:9Malango yake yamezama ardhini, makomeo yake ameyavunja na kuyaharibu. Mfalme wake na wakuu wake wamepelekwa uhamishoni miongoni mwa mataifa, sheria haipo tena, na manabii wake hawapati tena maono kutoka kwa Bwana. 10 2:10Wazee wa Binti Sayuni wanaketi chini kimya, wamenyunyiza mavumbi kwenye vichwa vyao na kuvaa nguo za gunia. Wanawali wa Yerusalemu wamesujudu hadi ardhini. 11 2:11Macho yangu yamedhoofika kwa kulia, nina maumivu makali ndani, moyo wangu umemiminwa ardhini kwa sababu watu wangu wameangamizwa, kwa sababu watoto na wanyonyao wanazimia kwenye barabara za mji. 12 2:12Wanawaambia mama zao, “Wapi mkate na divai?” wazimiapo kama watu waliojeruhiwa katika barabara za mji, maisha yao yadhoofikavyo mikononi mwa mama zao. 13 2:13Ninaweza kusema nini kwa ajili yako? Nikulinganishe na nini, ee Binti Yerusalemu? Nitakufananisha na nini, ili nipate kukufariji, ee Bikira Binti Sayuni? Jeraha lako lina kina kama bahari. Ni nani awezaye kukuponya? 14 2:14Maono ya manabii wako yalikuwa ya uongo na yasiyofaa kitu, hawakuifunua dhambi yako ili kukuzuilia kwenda utumwani. Maneno waliyokupa yalikuwa ya uongo na ya kupotosha. 15 2:15Wote wapitiao njia yako wanakupigia makofi, wanakudhihaki na kutikisa vichwa vyao kwa Binti Yerusalemu: “Huu ndio ule mji ulioitwa mkamilifu wa uzuri, furaha ya dunia yote?” 16 2:16Adui zako wote wanapanua vinywa vyao dhidi yako, wanadhihaki na kusaga meno yao na kusema, “Tumemmeza. Hii ndiyo siku tuliyoingojea, tumeishi na kuiona.” 17 2:17 Bwana amefanya lile alilolipanga; ametimiza neno lake aliloliamuru siku za kale. Amekuangusha bila huruma, amewaacha adui wakusimange, ametukuza pembe ya adui yako. 18 2:18Mioyo ya watu inamlilia Bwana. Ee ukuta wa Binti Sayuni, machozi yako na yatiririke kama mto usiku na mchana; usijipe nafuu, macho yako yasipumzike. 19 2:19Inuka, lia usiku, zamu za usiku zianzapo; mimina moyo wako kama maji mbele za Bwana. Mwinulie yeye mikono yako kwa ajili ya maisha ya watoto wako, ambao wanazimia kwa njaa kwenye kila mwanzo wa barabara. 20 2:20“Tazama, Ee Bwana, ufikirie: Ni nani ambaye umepata kumtendea namna hii? Je, wanawake wakule wazao wao, watoto waliowalea? Je, kuhani na nabii auawe mahali patakatifu pa Bwana? 21 2:21“Vijana na wazee hujilaza pamoja katika mavumbi ya barabarani, wavulana wangu na wasichana wameanguka kwa upanga. Umewaua katika siku ya hasira yako, umewachinja bila huruma. 22 2:22“Kama ulivyoita siku ya karamu, ndivyo ulivyoagiza hofu kuu dhidi yangu kila upande. Katika siku ya hasira ya Bwana hakuna yeyote aliyekwepa au kupona; wale niliowatunza na kuwalea, adui yangu amewaangamiza.” 3 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 31 3:1Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake. 2 3:2Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru; 3 3:3hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa. 4 3:4Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu. 5 3:5Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu. 6 3:6Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa. 7 3:7Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito. 8 3:8Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu. 9 3:9Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu. 10 3:10Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni, 11 3:11ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada. 12 3:12Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake. 13 3:13Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake. 14 3:14Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa. 15 3:15Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo. 16 3:16Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini. 17 3:17Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini. 18 3:18Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.” 19 3:19Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo. 20 3:20Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu. 21 3:21Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini. 22 3:22Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe. 23 3:23Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu. 24 3:24Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.” 25 3:25 Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta; 26 3:26ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana. 27 3:27Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana. 28 3:28Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake. 29 3:29Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini. 30 3:30Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu. 31 3:31Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele. 32 3:32Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu. 33 3:33Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu. 34 3:34Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi, 35 3:35Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana, 36 3:36kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya? 37 3:37Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru? 38 3:38Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema? 39 3:39Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake? 40 3:40Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu. 41 3:41Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme: 42 3:42“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe. 43 3:43“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma. 44 3:44Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya. 45 3:45Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa. 46 3:46“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu. 47 3:47Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.” 48 3:48Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa. 49 3:49Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu, 50 3:50hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona. 51 3:51Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu. 52 3:52Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege. 53 3:53Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe; 54 3:54maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali. 55 3:55Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo. 56 3:56Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.” 57 3:57Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.” 58 3:58Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu. 59 3:59Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu! 60 3:60Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu. 61 3:61Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu: 62 3:62kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa. 63 3:63Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao. 64 3:64Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda. 65 3:65Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao! 66 3:66Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana. 4 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 41 4:1Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara. 2 4:2Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi! 3 4:3Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani. 4 4:4Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye. 5 4:5Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu. 6 4:6Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada. 7 4:7Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi. 8 4:8Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo. 9 4:9Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani. 10 4:10Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa. 11 4:11 Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake. 12 4:12Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu. 13 4:13Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki. 14 4:14Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao. 15 4:15Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.” 16 4:16 Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki. 17 4:17Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa. 18 4:18Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika. 19 4:19Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani. 20 4:20Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa. 21 4:21Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi. 22 4:22Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako. 51 5:1Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu. 2 5:2Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni. 3 5:3Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane. 4 5:4Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua. 5 5:5Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko. 6 5:6Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha. 7 5:7Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao. 8 5:8Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao. 9 5:9Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani. 10 5:10Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa. 11 5:11Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda. 12 5:12Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima. 13 5:13Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni. 14 5:14Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao. 15 5:15Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo. 16 5:16Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi! 17 5:17Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia, 18 5:18kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake. 19 5:19Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi. 20 5:20Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu? 21 5:21Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale, 22 5:22isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.